Judges 3:12-17

12 aWaisraeli wakafanya maovu mbele za Bwana tena, kwa kuwa walifanya maovu hayo Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli. 13 bEgloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende
Yaani Yeriko.
14 dWaisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.

15 eWaisraeli wakamlilia tena Bwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi. 16Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye ukatao kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja,
Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45.
akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume.
17 gAkamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana.
Copyright information for SwhKC